ads slot

Latest Posts:

Kiongozi wa upinzani uganda atiwa mbaroni kwa kosa la kujitangazi mshindi

Kiongozi wa upinzani nchini Uganda,  Kizza Besigye ameshtakiwa kwa kosa la uhaini baada ya kujitangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika hivi karibuni.

Alikamatwa baada ya kuandaa sherehe zake mwenyewe za kuapishwa kabla ya sherehe za kuapishwa kwa Rais Yoweri Museveni
aliyechaguliwa kwa muhula wa tano.

Kiongozi huyo amekuwa kizuizini muda mwingi tangu February mwaka huu. Rais Museveni amekanusha madai ya kuiba kura.

Ulinzi ulikuwa umeimarishwa kwenye sherehe za kuapishwa kwa Museveni Alhamis iliyopita ikiwa pamoja na kuzuiliwa kwa maandamano ya upinzani.

Serikali iliwaonya waandishi habari kutoripoti maandamano yoyote.

Mitandao ya kijamii kama vile Whatsapp, Facebook na Twitter
Ilizuiliwa kwa agizo la serikali ikidai ni sababu za kiusalama.

Bonyeza
Share on Google Plus

About felkiul

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment